Posts

Showing posts from June, 2022

JINSI YA KUONDOA CHUNUSI USONI

Image
 🍅UREMBO ASILI🍅 SEHEMU YA KWANZA,  🍎JINSI YA KUTOA CHUNUSI SUGU USONI NA MIKUNJO YA NGOZI. MAKOVU NA  KUONDOA TATIZO LA NGOZI KUWA KAVU VILEVILE MCHANGANYIKO HUU UNAFAA KWA WALE WENYE MAFUTA USONI🍅 KARIBU NIKUJUZE HUSIYOYAJUA NA KAMA UNAYAJUA BASI NAKUONGEZA UJUZI.. KAMA UNAVYOONA KWENYE PICHA HAPO👇🏻 KUNA LIMAU 🍋 KUNA YAI 🥚 NA ASALI MBICHI YA NYUKI🐝 BILA SHAKA VITU VYOTE IVI VINAPATIKANA KWA URAHISI SANA VILE VILE  HAVICHUKUI MUDA MREFU SAANA 👇🏻 KUVIANDAA👇🏻 TUPATE CHOMBO KISAFI YAWEZA KUWA BAKURI AU KIFAA CHOCHOTE CHUKUA YAI LA KUKU KAMA UTAPATA YAI LA KIENYEJI ITAPENDEZA ZAIDI  LIVUNJE KATI TUNACHOHITAJI.KWENYE YAI NI ULE UTE MWEUPE KAMA MAJI SIO KIINI CHA NJANO👇🏻   BAADA YA HAPO CHUKUA LIMAO KAMLIA MAJI YA LIMAO  KIDOGO SAANA KWA SABABU LIMAO NI NZURI KWA NGOZI LAKINI UKIWEKA NYINGI ITAKUWASHA USONI WEKA KIDOGO TU👇🏻 Chukua na asali kijiko kimoja weka kwenye mchanganyiko wako wa yai na lamao  baada kuweka asali tumia kijiko kuchanganya vitu vyako koroga vizuri 👇🏻 Su

DAWA YA KUTIBU VIDONDA VYA TUMBO HATA KAMA VIDONDA NI SUGU

Image
  MAHITAJI HABATI SODA YA UNGA VIJIKO 4 KOMA MANGA YA UNGA VIJIKO 4 MDALASINI WA INDIA WA UNGA VIJIKO 4 ASALI MBICHI NUSU LITA CHUKUA DAWA HIZO ZOTE  ZICHANGANYE SEHEMU MOJA BAADA YA KUZICHANGANYA SEHEMU MOJA CHANGANYA NA ASALI MBICHI NUSU LITA  HAKIKISHA UMECHANGANYA VIZURI DAWA YAKO  BAADA YA HAPO ANZA MATUMIZI YA DAWA KUNYWA VIJIKO 2 X 2 KWA SIKU  KWA MAANA HIYO UNAKUNYWA HASUBUI VIJIKO VIWILI NA JIONI VIJIKO VIWILI KWA MUDA WA SIKU 10 Dawa hii ndo mwisho wa tatizo la vidonda vya tumbo  KWA IDHINI YA ALLAH UTAPONA BAADA YA KUPONA MSHUKURU ALLAH S.W SIO DR.ABDALLAH MIMI NIMEKUFUNDISHA HASIBAB TU TABIBU NI ALLAH.

TIBA YA KUKOJOA KITANDANI KWA MTU MZIMA NA WATOTO

Image
 JE,TATIZO LA MTU MZIMA KUKOJOA KITANDANI(ADULTS NOCTURNAL ENURESIS) NI NINI? Hili ni tatizo linaowasumbua watu wengi walio katika umri ambao tayari wana uwezo wa kuzuia mkojo,tatizo hili hutokea kwa mtu huyo ambaye tayari yupo katika umri wa kuweza kujizuia mkojo ila anakua bado anaendelea kukojoa kitandani au kwenye nguo. Hivyo tunaweza kusema hili ni  tatizo la kushindwa kuzuia mkojo wakati wa mchana au usiku na linalotokea katika umri wa miaka mitano au zaidi. Mkojo unapo hifadhiwa katika kibofu cha mkojo, kibofu kinatanuka kama puto. Katika sehemu za neva za kutanua kuta za kibofu cha mkojo zinapeleka ishara ya kuzuia mkojo katika akili. Hii hutokea katika sehemu ya ubongo inayohusika na matendo yasiyo ya hiari. Kama ubongo wa mtoto haujapata ishara hii, au ukishindwa kujua maana ya hiyo ishara, hatua ya makusudi ya kuzuia mkojo haitafanyika hivyo mtu hushindwa kupata uwezo wa kuxuik mkojo. Hali hii mara nyingi husababishwa na kuchelewa kwa ukuaji wa kibiologia wa utendaji kazi wa

FAIDA ZA MAFUTA YA MLONGE

Image
  FAIDA ZA MAFUTA YA MLONGE _huondoa vipele kwenye ngozi. _hutibu homa za mara KWA mara. _huondoa malaria sugu. _huondoa vitambi kwa akina mama. Na akina baba. _hupunguza mtu kuwa na hasira. _hulainisha ngozi. _kukuza nywele na kuzifanya ziwe nyeusi. _huondoa uchovu. _hutibu fangasi. _huondoa mabaka na michubuko. _huondoa ukurutu. _huondoa harufu mbaya sehemu za siri. _hutibu tatizo la mchafuko wa damu (allergy).. _huongeza CD4 mwilini. Ambazo zikipungua ni rahisi sana kupata virusi vya VVU  kwaiyo ni vizuri mtu akanywa mafuta ya MLONGE au kutafuna mbegu  zake. _kutibu kisukari. _hutibu kuhara damu. _huondoa uvimbe tumboni  _huongeza kasi ya utokaji mkojo kwa wale wenye matatizo ya mkojo  unaotoka kidogo kidogo. _ _hutibu presha ya kupanda na kushuka. _hutibu pumu. _hutibu maradhi yote ya MOYO. _ huondoa tatizo la ugumba.(kutoshika mimba) _huondoa uvimbe kwenye mfuko wa uzazi. _huongeza nguvu kiume na kike. _huondoa mawe kwenye kibofu cha mkojo. _hutibu fangasi za ndani ya damu. _hutib

TIBA YA SARATANI KWA KUTUMIA STAFELI

Image
 Allah s.w hakika ameweka ponyo kwenye mti huu wa mstafeli mti huu unazungumziwa sana nchini kwa sababu umewasaidia watu wengi katika kuwatibu magonjwa sugu hasa ugonjwa huu unaowasumbua watu saratani ya #tezi dume na saratani nyingine nyingi.  Saratani aina zote zinatibika kwa kutumia mstafeli. Kama vile_ Saratani ya mapafu. Saratani ya mdomo. Saratani ya kwenye ulimi. Saratani ya shingo ya kizazi. Saratani ya ini.. Saratani ya mji wa uzazi. Saratani ya matiti . Saratani ya kongosho. Na nyingine nyingi. Majani ya mstafeli yanatibu. Maumivu ya mgongo. Kisukari. Yanaongeza kinga ya mwili. Yanaimarisha afya ya mfumo wa upumuaji. Mazuri kwa afya ya moyo. Maumivu ya nyonga. Yanaongeza cd4 mwilini nk.. Matumizi unaweza kutengeza juice yake kwa kutumia matunda yake ukawa unakunywa glas moja x 2 kwa siku. Kwa muda wa siku 21  au ukachemsha majani yake  ukawa unakunjwa kikombe kimoja x2 kwa siku kwa muda wa siku 21 Kama hauwezi hayo yote basi chukua majani ya mstafeli yaponde au yatwange kisha

MAUMIVU YA KICHWA NA TIBA YAKE

Image
 MAUMIVU YA KICHWA NA TIBA YAKE   Ukihisi Maumivu Ya Kichwa Unafaa Kufanya Nini? 1• achana na mawazo 2 • epuka vilevi vyote 3• oga/ koga maji ya moto 4• kula vyakula vya asili 5• kuwa mtulivu 6• pata kupumzika 7• kunywa maji ya kutosha kila siku 8• epuka vyakula kama siagi ya karanga, chokoleti, chai ya rangi, kahawa na soda 9• tumia zaidi vyakula vyenye Vitamini C, Vitamini B2 na madini ya magnesium 10• fanya masaji ya kichwa, ya shingo na ya mgongo Vilevile unaweza pia kutumia vitu vinavyopatikana nyumbani Kumbuka maumivu yakizidi muone daktari kwa uchunguzi zaidi. @-SHURUBATI YA MNANAA  Dawa nyingine ya asili ya kutibu maumivu ya kichwa ni juisi ya mnanaa kwa kuwa mnanaa una vitu vya kutoa maumivu ya kichwa vijulikanavyo kama ‘menthol’ na ‘menthone’. Pia unaweza kutumia mvuke uliotokana na chai ya majani ya mnanaa ujifunikie sehemu ya mbele ya kichwa chako. @-TANGAWIZI  Inachofanya tangawizi ni kupunguza maambukizi kwenye mishipa yako ya damu. Kuna namna mbili unaweza kutumia tangaw

TIBA KWA KUTUMIA KARAFUU

Image
 TIBA KWA KUTUMIA KARAFUU karafuu ni miongoni mwa kiungo cha chakula na dawa mbali mbali karafuu inajulikana ulimwenguni kwa tiba  magonjwa mbali mbali. Magonjwa hayo ni kutoa gesi tumboni, tatizo la mmeng'enyo.kutapika, na matatizo katika meno. JITIBU KWA KUTUMIA KARAFUU Matatizo katika misuri #ganzi ya mikono na miguu. #kiharusi  #maumivu ya viungo. #uvimbe. Tumia mafuta ya karafuu kwa kuchulia sehemu yenye matatizo. . #KUHARISHA Chukua karafuu weka kwenye maji chemsha kunywa kuharisha kutaisha  #KICHEFUCHEFU tafuna punje za karafuu  tatu kichefuchefu kitaisha. #MATATIZO #YA #MENO Sukutua maji ya uvugu  vugu yalichemshwa na karafuu. #MAUMIVU YA KICHWA.(kipanda USO) Chukua mafuta ya karafuu changanya na chumvi ya mawe kidogo kisha pakaa kichwan sehemu inayouma. Maumivu yata kata. #JINO LILILOTOBOKA:    chukua pamba weka ktk mafuta ya karafuu kisha weka kwenye jino lililotoboka ukiweka iyo pamba sikilizia kama dakika 30 ndo uitoe Fanya ivyo kwa wiki mala 3 utaona matokeo mazuri ins

UGONJWA WA BAWASIRI AU KUOTA KINYAMA SEHEMU YA HAJA KUBWA

Image
 UGONJWA WA BAWASIRI AU KUOTA KINYAMA SEHEMU YA HAJA KUBWA WATU  wengi wanasumbuliwa na tatizo hili ambalo huwafanya kuwa na uoga na aibu wa kuelezea na kushindwa hata kwenda hospital kupata tiba JE, UNAJUA BAWASIRI/HEMORRHOIDS NI NINI? Ni ugonjwa unaotokana na kuathirika kwa mishipa ya damu ya ndani na Inje ya sehemu ya haja kubwa na wakati mwingine mishipa hiyo huweza kupasuka/kuteleza na kuvuja damu kwenye njia ya haja kubwa na kasababisha kutoka kinyama au uvimbe. ugonjwa huu wa bawasiri kwa lugha ya kitaalamu tunauita HEMORRHOIDS ilhali kwa lugha ya kingereza unafahamika kama piles. Tatizo hili huwaathiri watu wote ila zaidi huwaathiri watu wazima kuliko watoto na inakadiriwa kuwa karibu 50%ya watu wote wako katika hatari ya kupata tatizo hili katika umri wa miaka 30 mpaka 50 AINA ZA BAWASIRI Kuna Aina kuu mbili za bawasiri Aina hii ya bawasiri hutokea ndani ya mfereji wa haja kubwa huwa haiambatani na maumivu na wengi huwa hawajitambui kuwa Wana tatizo hili Aina hii hutokana na k

FAHAMU KUHUSU KAROTI NA FAIDA ZAKE KIAFYA

Image
SOMO LETU  LEO TUNAJIFUNZA KUHUSU KAROTI. karoti ni moja wapo kiungo watu wanatumia karoti kuungia mboga na wengine wanatumia kutafuna tu lakini sina uhakika kama watu wanajua umuhimu wa karoti kwa afya  zao 👉Wataalamu wa tiba asili namimi nikiwemo wanashauri kuwa hili uwe na afya bora inabidi ule karoti 6 kwa wiki. Unaweza kula karoti kwa kuchemsha_ Kula mbichi au kunywa juce yake. 👉karoti husaidia kuondoa tatizo la macho kutoona vizuri usiku pia inasaidia kuondoa tatizo la #ALLERGY kwenye macho_ Mfano macho kuwasha sababu ya vumbi au moshi. 👉karoti inalekebisha seli mwilini na kuzifanya zisizeeke mapema hii ni kutokana vitamin A) iliyopo kwenye karoti. 👉karoti huifanya ngozi iwe nzuri na yenye kupendeza_ Kama unataka kutumia karoti hili kufanya ngozi yako ipendeze  iwe laini chukua asali mbichi kijiko 1 cha chakula  na mafuta ya mzaituni (olive oil)  kijiko kimoja cha chakula na maji ya limao kijiko kimoja vyote ivyo unachanganya kwenye juisi ya karoti nusu glas_ Changanya mchang

SABABU NA TIBA YA TUMBO KUJAA GESI

Image
 SABABU NA TIBA YA TUMBO KUJAA GESI. Tatizo la tumbo kujaa gesi husababishwa  na kumeza chakula pamoja na gesi inayotolewa katika vyakula mbalimbali tunavokula ambayo hujaa tumboni na kwenye utumbo mdogo. Hali hii husababisha tumbo kujaa au kuvimba na mtu hutoa gesi hiyo kwa njia ya ushuzi na kubeua.   NINI HUSABABISHA? Tatizo ili mara nyingi husababishwa na huambatana na mambo yafuatayo: 1. Kula vyakula vyenye mafuta mengi ambayo huchelewesha tumbo kufunguka kwa ajili ya usagaji wa chakula. 2. Kunywa vinywaji vyenye Carbonates, cola na kula vyakula vyenye gesi kama maharage, bigiji, vitunguu, kabichi n.k  3. Msongo wa mawazo na hasira 4. Kula haraka haraka na kula unaongea. 5. Uvutaji wa Sigara 6. Magonjwa na maambukizi katika mfumo wa chakula asa kwenye tumbo na utumbo ambayo huzuia kusagwa na kufyonzwa kwa chakula. TIBA YAKE  A-Kunywa chai ya tangawizi au karafuu itasaidia kupunguza gesi B-Unaweza kunywa glasi moja ya juisi ya Limao baada ya kula. C-Tafuna mbegu za maboga zinasaidia

UWEZO WA STAFELI KATIKA KUPAMBANA NA MAGONJWA SUGU

Image
 UWEZO WA STAFELI KATIKA KUPAMBANA NA MAGONJWA SUGU @-Stafeli ni tunda lenye faida lukuki kwa afya ya mwanadamu. Zifuatazo ni faida muhimu za mti wa Mstafeli. @-KWA mfano baadhi ya dawa za hospitali huathiri njia ya chakula na kumsababishia mgonjwa ukosefu wa choo kwa muda mrefu, lakini stafeli likitumika hurekebisha hali hiyo na kumsaidia mgonjwa kupata choo kama kawaida. @-Vilevile, baadhi ya dawa za hospitali za saratani hudhoofisha kinga ya mwili, lakini virutubisho vilivyomo kwenye stafeli, hasa vitamin C, huzifanya kinga kuwa imara na hivyo kuziimarisha hivyo kumuepusha mtu kupatwa na maambukizi mengine, kama ya njia ya mkojo, mafua na kikohozi cha mara kwa mara. FAIDA ZINGINE ZA STAFELI NI KAMA ZIFUATAVYO: Hutoa nafuu ya kipanda uso. Kirutubisho aina ya Riboflavin kilichomo kwenye stafeli, husadia kutoa nafuu kwa ugonjwa wa kichwa cha kipanda usoni. 1- HUZUIA UGONJWA WA ANEMIA Madini ya chuma (iron) yaliyomo kwenye stafeli, hufaa sana katika kuzuia ugonjwa wa kukauka damu mwilin

ZIJUE FAIDA KUMI ZA ASALI KIAFYA.

Image
 ZIJUE FAIDA KUMI ZA ASALI KIAFYA. Kwa miaka mingi asali imekuwa ikitumika kiafya kwa ajili ya tiba asili ya magonjwa na matatizo mbali mbali kama maambukizi, kuungua, vidonda, makovu, uvimbe na maumivu. Zifuatazo ni faida kumi za asali kiafya:- 1. Asali ikichanganywa na maziwa usaidia kupunguza kiungulia. 2. Mchanganyiko wa asali na Limao kwenye chai husaidia kutibu kikohozi na maambukizi kwenye mfumo wa hewa. 3. Mchanganyiko wa asali na tangawizi huzuia kutapika kwa mgonjwa na mama mjamzito. 4. Asali ina kemikali za flavonoid na antioxidants zinazosaidia kuzuia magonjwa ya moyo na saratani. 5. Asali ina kemikali ya hydrogen peroxide ambayo husaidia kuua bakteria na fungasi mwilini. 6. Huwasaidia wanariadha kuongeza nguvu na kupata ahueni mapema kila baada ya kukimbia kwani ina kiasi kikubwa cha glycogen. 7. Asali huongeza kinga ya mwili kwa kuraisisha mfumo wa chakula na damu kufanya kazi vizuri. 8. Mchanganyiko wa asali na juice ya machungwa husaidia kuondoa sumu mwilini na kuimaris

TIBU MAGONJWA YA/NA PRESSURE YA MACHO (GLAUCOMA

Image
 EPUKA UPOFU: TIBU MAGONJWA YA/NA PRESSURE YA MACHO (GLAUCOMA) Ugonjwa wa macho huathiri mishipa ya fahamu inayohusika na kuona kitaalamu huitwa optic nerve na mgonjwa asipokua makini na matibabu yake basi huweza kupata upofu wa moja kwa moja na asione tena maishani mwake. MAGONJWA HAYO NI KAMA ; 1-Pressure ya macho (Glaucoma), Ugonjwa wa macho unaosababishwa na Kisukari (Retinopathy), 2-Macho makavu, Tongotongo (Mucus), Wekundu wa macho (Red Eyes), 3-Uvimbe wa macho na mishipa ya macho na (Uveitis) kusababisha uharibifu wa tishu za macho, 4-Uchovu wa macho utokanao na kuangalia miale na mwanga mkali, Tv (Eyestrain), Upofu Wa Usiku (Nyctalopia), 5-Mtoto Wa Jicho, Mtazamo Wa Karibu (Myopia & Hypermetropia), Ugonjwa wa jicho unaohusishwa na kuzeeka (Presbyopia), Strabismus (au Msalaba Macho), nk CHANZO CHA UGONJWA Kitaalamu upande wa mbele ya jicho kuna majimaji ambayo kitaalamu tunaita aquous homour ambayo kazi yake ni kuleta virutubisho kwenye sehemu za jicho iitwayo iris, lenzi na

JIFUNZE JINSI YA KUTIBU MAUMIVU YA SIKIO KWA KUTUMIA KITUNGUU SAUMU

Image
  JIFUNZE JINSI YA KUTIBU MAUMIVU YA SIKIO KWA KUTUMIA KITUNGUU SAUMU Tatizo la kuumwa sikio linajitokeza mara kwa mara katika jamii zetu, ni tatizo lakawaida lakini huwa hatari zaidi hasa pale tiba inapopuuzwa au kucheleweshwa          SABABU ZAKE Miongoni mwa sababu za kupata maumivu makali ya sikio ni:-  1. Maambukizi yatokanayo na bakteria, fangas, virus n.k  2. Kubadilika kwa mkandamizo wa presha(pressure changes) kwenye masikio mfano wakati wa kuogelea na shughuli zingine  3. Maji kuingia masikioni  4. Hali ya hewa  iliyoptiliza  5. Kuchokonoa masikio            TIBA Menya kitunguu saumu kisha kamua juice yake, ipashe moto kiasi kisha itumike ikiwa bado ya vuguvugu. Usichanganye na maji          DOZI Dondoshea matone 2 - 3 ya mafuta hayo(juice) katika sikio lenye tatizo kisha weka pamba ama kitambaa safi kwa muda wa dakika 30 kufanya dawa iendelee kuwepo sikioni.... Fanya hivyo kwa muda wa siku 2 hadi 3 tatizo litaisha   ZINGATIA  1. Tumia dawa ikiwa ya vuguvugu(sio ya moto sana

FIGO NA UTENDAJI WAKE

Image
Figo Zipo mbili zinapatikana upande wa chini wa uti wa mgongo. Damu inapita katika figo na kurudia rudia figo, figo inasafisha na kuchuja damu,  figo inatenganisha damu na uchafu na sumu mbali mbali. Damu safi inasambaa mwilini uchafu unatoka kwa NJIA ya haja ndogo (MKOJO) Figo inasimamia kiwango cha maji pia. Pia figo inazalisha MKOJO Lita 2 kwa siku, kazi nyingine ya figo ni kusababisha uwekundu katika damu  na kulinda uwekundu usipotee. MAWE KATIKA FIGO Mawe yanatokea katika figo kutokana na mahambukizi ya figo. Kuzuia kuingia MKOJO katika kibofu kunasababisha MATATIZO katika kibofu, MKOJO unaganda na kusababisha mawe. Kutokula vyakula vyenye vitamin na lishe vinasababisha MKOJO kuwa mzito na kutengeneza vijiwe. Vyakula vya asidi na kutokunywa maji kwa wingi ni sababu ya mawe katika figo, kutumia vyakula vyenye sukari nyingi vinasababisha mawe katika kibofu. DALILI ZA MAWE KATIKA FiGO _kukojoa damu au usaha _maumivu wakati wa kukojoa. _maumivu katika kibofu na kwenye kiuno na maeneo

FAHAMU KUHUSU TEZI DUME.

Image
Kila mwanaume anazaliwa na Tezi ya kiume. Tezi dume siyo ugonjwa bali ni kiungo kama viungo vingine mwilini. Tezi dume inapatikana katika mfumo wa uzazi wa mwanaume katika shingo ya kibofu cha mkojo. Kazi yake kubwa nikutengeneza majimaji ya uzazi wa mwanaume (shahawa), ambayo husaidia kurutubisha mbegu za kiume zilizo tengenezwa kutoka kwenye Korodani; na husaidia mbegu za kiume kubaki hai kwa muda unaostahili. Tatizo linakuja kiungo hiki kinapoanza kutanuka. Kiungo hiki kinatanuka taratibu taratibu mnoo. Hili ni tatizo linalo wakumba wanaume wengi. Takwimu zinaonesha kwamba kati ya wanaume 10, wa 5 na kuendelea wana dalili za kutanuka kwa Tezi dume. Ukuwaji wa Tezi dume ni ile hali ya chembe chembe hai katika tezi ya kiume kukua bila kufuata utaratibu wa mfumo wa mwili katika eneo linalo zunguka mirija ya kupitisha mkojo na mbegu za kiume.  Tatizo hili kwa sasa linawapata wanaume kuanzia umri wa miaka 25 na kuendelea, tofauti na awali lilikuwa miaka zaidi ya 50. Takwimu kutoka kwenye

FAHAMU KUHUSU UGONJWA WA PUMU

Image
                   #PUMU__ ni miongoni mwa ugonjwa sugu unaowasumbua watu duniani. Neno PUMU maana yake in ugumu wa upumuaji katika hali ya kawaida, mgonjwa hupumua  kwa mdomo au pua, kupitia katika mirija ya hewa na kusafiri_ Katika mapafu. MTU mwenye afya upumua kwa sekunde 16 adi 18 watoto sekunde 20 adi 25 watoto wachanga sekunde 40 ,  _ MTU mzima huvuta hewa 230 adi 250 za sentimenta za mraba za hewa , lakini kwa mgonjwa wa PUMU sivyo hivyo zaidi ya kupumua kwa shida na sauti kukoroma. AINA_ZA_UGONJWA_WA_PUMU KUNA AINA MBILI ZA UGONJWA WA PUMU. 1)PUMU ya kikoromeo inaitwa hivyo kwa sababu tatizo linatokea katika koromeo. 2)PUMU ya moyo(cardiac asthma) matatizo yanatoka katika moyo kutoweza kupumua vizuri kwa sababu ya kuferi kwa moyo. SABABU_ZA_KUPATA_PUMU 1) Mzio(allergy) UGONJWA wa PUMU unasababishwa na mzio. Mzio ni aina ya mkatazo katika mwili  , mzio unaweza kuwa wa manukato mbali mbali ,vumbi ,na vyakula mbali mbali mfano watu wengi wana mzio wa maziwa,mayai , na baadhi ya s

FAHAMU KUHUSU UGONJWA WA KISUKARI

Image
  LEO KWENYE SOMO LETU TUNAJIFUNZA KUHUSU UGONJWA WA KISUKARI. Chanzo cha ugonjwa wa kisukari. Dalili za ugonjwa wa kisukari. Tiba za ugonjwa wa kisukari. Kwa kutumia njia za asili. Karibu sana. #ZAMANI ugonjwa huu watu walikua wanauita  mkojo mtamu . sukari nyingi mwilini kuliko kawaida_ Ya mahitaji katika mwili wa binadamu  japo kuwa kuna ugonjwa wa upungufu wa sukari . sukari inakua nyingi kwakua inachujwa na kuingia katika mfumo wa mkojo_ Wakati wa damu inapopita katika figo na mkojo wa mgonjwa kuwa mtamu. Kuwemo kwa sukari nyingi mwilini au katika damu  kutokana na kuyeyushwa kwa vyakula vya wanga kwa mfano. Ugali ,wali, mkate nk..kuyeyushwa  ili ikatumike kuleta joto mwilini_ Na kutia nguvu mwilini . ulaji wa vitu vitamu bandia, pombe ,kahawa,bickuti,sigara na soda aina zote.  Hivi ni vitu vinavyosababisha sukari kuwa nyingi mwilini_ Sukari hurundikana katika damu  kwa kukosa kwa kwenda kwa sababu ya upungufu wa homoni ya #INSULIN upungufu waweza kuleta maradhi yanayozingira kong

adthis