FAHAMU KUHUSU KAROTI NA FAIDA ZAKE KIAFYA



SOMO LETU  LEO TUNAJIFUNZA KUHUSU KAROTI.


karoti ni moja wapo kiungo watu wanatumia karoti kuungia mboga na wengine wanatumia kutafuna tu lakini sina uhakika kama watu wanajua umuhimu wa karoti kwa afya  zao


👉Wataalamu wa tiba asili namimi nikiwemo wanashauri kuwa hili uwe na afya bora inabidi ule karoti 6 kwa wiki. Unaweza kula karoti kwa kuchemsha_


Kula mbichi au kunywa juce yake.


👉karoti husaidia kuondoa tatizo la macho kutoona vizuri usiku pia inasaidia kuondoa tatizo la #ALLERGY kwenye macho_


Mfano macho kuwasha sababu ya vumbi au moshi.


👉karoti inalekebisha seli mwilini na kuzifanya zisizeeke mapema hii ni kutokana vitamin A) iliyopo kwenye karoti.


👉karoti huifanya ngozi iwe nzuri na yenye kupendeza_


Kama unataka kutumia karoti hili kufanya ngozi yako ipendeze  iwe laini chukua asali mbichi kijiko 1 cha chakula  na mafuta ya mzaituni (olive oil)  kijiko kimoja cha chakula na maji ya limao kijiko kimoja vyote ivyo unachanganya kwenye juisi ya karoti nusu glas_


Changanya mchanganyiko wako vizuri kisha tumia  sugua taratibu sehemu yoyote ya ngozi unayotaka ipendeze kisha kaa kama muda wa dakika 15 ndo uwende kuoga au kunawa kwa maji ya kawaida tiba hii ni nzuri sana itakusaidia kuondoa chunusi mba,mabaka, na kuondoa madoa doa kwenye ngozi yako.


👉karoti husaidia kuondoa sumu (taka) mwilini na kuondoa mafuta yasiyotakiwa mwilini na kusafisha njia ya haja kubwa na kusaidia kupata choo vizuri.


👉karoti zinasaidia fizi na meno kuwa amara na kuchochea uzalishaji wa mate.


👉karoti inasaidia kuzuia kiharusi utafti unaonyesha  kuwa ulaji wa karoti 6 kwa wiki husaidia kutopata kiharusi.


👉karoti husaidia kuondoa tatizo la shinikizo la damu.


👉karoti husaidia tatizo la kupoteza kumbu kumbu. (Kusahau)


👉ulaji wa karoti 6 kwa wiki zinasaidia kutopata ugonjwa saratani bi maana karoti zinatumika kama kinga ya ungonjwa wa saratani na ugonjwa wa kisukari. Nk..


👆hizo ndo faida za kula karoti. Tujitahidi sana kula angalau karoti 6 kwa wiki

Comments

adthis

Popular posts from this blog

FAIDA ZA PILIPILI MANGA KIAFYA

FAHAMU FAIDA 10 ZA NAZI KAMA TIBA YA MWILI