FAIDA SABA (7) ZA MDALASINI (CINNAMON)


Mdalasini ni aina ya mmea ambao hutumika kama kiungo kwenye chakula kwani hutia radha madhubuti kutokana na harifu yake nzuri ya kuvutia.

Faida zake

1.KUPUNGUZA KOLESTEROLI MBAYA MWILINI.
Kolesteroli/lehemu (cholesterol) ni aina ya mafuta/fati (fat) ambayo hupatikana kwenye chembe za damu.kolestroli huwa ni kama nta ambayo wakati mwingine hujishikiza kwenye kuta za mishipa ya damu. Hii ni kwa sababu ya vyakula vyenye mafuta(lipid foods) kama nyama n.k. Hivyo mdalasini hupambana na cholesterol/lehemu aina ya lipoprotini ya chini LDL(Low Density Lipoprotein) ambayo husabaisha shinikizo la damu (hypertension).


2. MDALASINI HUWA NA VIRUTUBISHO MUHIMU KWA MWILI.
 Virutubisho hivyo huwa kazi kama kuboresha mifupa na meno kuwa imara zaidi yaani meno huwa na kinga dhidi ya kuoza


3.KUSAIDIA KUPUNGUZA UZITO.
Kwa matumizi mfululizo ya mdalasini husaidia kupunguza uzito usiostahili


4. MDALASINI HUWA NA KAZI YA KUBORESHA KIWANGO CHA SUKARI KWENYE DAMU. Kumbuka kiwango cha sukari kikiwa juu sana au chini sana husababisha kisukari(diabetes)



5.KUZUIA MAUMIVU YA VIUNGO (ARTHRITIS)
Tatizo la maumivu ya viungo hutokea pale mtu akiwa amepatwa na mshituko kwenye maungio. Pia kwa wale wenye maumivu yatokanayo na umri (uzee)


6.KUZUIA SELI ZA MWILI KUHARIBIKA(ANTIOXIDANTS)
Huongeza nguvu katika seli za mwili na ufanyaji kazi wake.


7.KUZUIA FANGASI NA BACTERIA. Fangasi na bakteria huchafua damu na kusababisha magonjwa ya ngozi na kuoza kwa meno. Hivyo mdalasini huzuia fangasi na bakteria


8.KUZUIA SARATANI YA TUMBO.
 Kutokana na kuongeza kinga dhidi ya magonjwa


8.KUTIBU KIFUA NA HOMA.
Husaidia kusafisha mfumo wa upumuaji (hewa)

🥝🥝Tumia Mdalasini kwa Vykula Na hata Vinywaji Ujijengee Afya bora na Kujiweka Pazuri

Comments

  1. thanks
    unaweza kusoma kitabu cha mboga na matunda hapa
    http://www.bongoclass.com/maktaba/matundab.html

    ReplyDelete

Post a Comment

adthis

Popular posts from this blog

FAIDA ZA PILIPILI MANGA KIAFYA

FAHAMU FAIDA 10 ZA NAZI KAMA TIBA YA MWILI