Posts

Showing posts with the label simulizi

KISA CHA MWANAFUNZI ROSE

Image
Kuna mwalimu wa shule ya sekondari alikuwa amezoea kumchapa viboko mwanafunzi mmoja mchelewaji. Mwanafunzi huyu alikuwa akichelewa kipindi cha kwanza kila siku. Hivyo, siku ambazo mwalimu huyu alikuwa na kipindi cha kwanza, mwanafunzi huyu alikuwa anachapwa kwanza kabla ya kuingia darasani. Hali hii iliendelea kwa muda mrefu. Wiki moja ilipita bila yule mwanafunzi kuonekana shuleni. Wiki lililofuata yule mwanafunzi alifika shuleni kabla ya mwanafunzi mwingine yeyote. Mwalimu yule alipomwona alifurahi sana. Alipoingia darasani alimwita yule mwanafunzi na kumsifia sana mbele ya darasa. "Rose, simama. Darasa, Mpigieni makofi "Rose" kwa sababu leo kawa wa kwanza kufika shuleni. Kumbe fimbo zile zimesaidia enhe" Wanafunzi walipiga makofi huku wengine wakimcheka huyo "Rose" Yule mwanafunzi alimwomba mwalimu ampe nafasi aseme jambo. Mwalimu akamruhusu "Mwalimu, siku zote nilizokuwa nikichelewa kufika shule nilikuwa namuuguza mama yangu. Baba yang...

MKE WANGU SAMAHANI (FULL STORY)

Image
MKE WANGU SAMAHANI             (FULL STORY) Asubuhi aliamka na kumkuta mkewe akisali. Akamsikia mkewe akimuombea. Akamtazama kwa sekunde kadhaa. Ni muda mrefu sana tokea amemshuhudia mkewe akisali. Wamekuwa na ugomvi na kutoelewana katika ndoa yao Kwa miezi kadhaa sasa. Usiku wa jana yake wamegombana ugomvi mkubwa mno. Haraka haraka Mume akainuka kitandani na kuelejea jikoni kuandaa kifungua kinywa. Kwa hio miezi kadhaa ya ugomvi mkewe amekua hamuandalii chakula. Kwa mshangao, akakuta staftahi imeshaandaliwa mezani. Akala. Baada ya kumaliza akarudi chumbani, kujiandaa aingie bafuni. Mke nae akawa anatoka bafuni. "Habari za asubuhi. Uwe na siku njema". Mke akamsalimia mumewe na kumtakia kazi njema, huku wakipishana bafuni Baada ya kuoga, na kuvaa tayari kwenda kazini; akamuona mkewe jikoni, akila staftahi akiwa na amani. Alikuwa akila kifungua kinywa huku akicheka kutokana na kuangalia video za vichekesho alizotumiwa WatsApp. Mume akamtizama k...

adthis