Posts

Showing posts from December, 2019

Dondoo Za Afya

FAIDA ZA TANGO 1. Kuzuia kisukari, kuboresha mfumo wa damu na kuondoha kolesteroli mwilini. 2. Chanzo kikubwa cha Vitamin B. 3. Kusaidia kutunza ngozi. 4. Kuongeza maji mwilini. 5. Kukata hangover. 6. Kuimarisha mmeng'enyo wa chakula mwilini. 7. Kuzuia saratani mwilini. 8. Kusaidia kupungua uzito. 9. Kuondoa maumivu na kuboresha viungo vya mwili. 10. Kuondoa harufu mbaya ya kinywa. FAIDA ZA PAPAI 1. Kuua na kuondoa mazalia ya minyoo mwilini. 2. Kusaidia kutibu vidonda vya tumbo. 3. Kuboresha mmeng’enyo wa chakula. 4. Majani yake huleta ahueni kwa wagonjwa wa saratani. 5. Kupunguza uvimbe (anti-inflammatory). 6. Kuboresha misuli na neva mwilini. 7. Kusaidia kumeng’enya protini. 8. Kuboresha kinga ya mwili. 9. Kuboresha macho. 10. Kuboresha mfumo wa hewa FAIDA ZA UBUYU 1. Kuzuia uhalibifu na mikunjo ya ngozi. 2. Kusaidia katika kupunguza uzito wa mwili. 3. Kuimarisha moyo. 4. Kusafisha ini na kuondoa sumu. 5. Kiwango kikubwa cha vitamin C. 6. Chanzo cha m

FAHAMU KUHUSU VIDONDA VYA TUMBO.

Image
VIDONDA VYA TUMBO,DALILI NA MATIBABU YAKE VIDONDA VYA TUMBO NINI?? >Ni kuharibika kwa ukuta wa tumbo la chakula na sehemu ya mwanzo ya utumbo mwembamba Kuna aina kuu mbili za vidonda vya tumbo 1. Gastric ulcers-hivi hutokea kwenye mfuko wa tumbo la chakula 2. Duodenal ulcers-hivi hutokea sehemu ya mwanzo ya utumbo mwembamba VISABABISHI VIKUU VYA VIDONDA VYA TUMBO 1. KUONGEZEKA KWA TINDIKALI YA HCL KWENYE TUMBO LA CHAKULA >imekuwa ni changamoto kubwa sana kwani moja ya visababishi hivi kila siku tunakumbana navyo ndiyo maana kwa nchi kama Tanzania kutibu vidonda vya tumbo ni changamoto kubwa. VIFUATAVYO HUONGEZA TINDIKALI YA HCL A. Mawazo Watu wengi tunasumbuliwa na changamoto hii ya kushambuliwa na msongo wa mawazo kila siku hii inatokana na kutojua namna ya kushughulika na msongo wa mawazo. Jifunze namna ya kuepuka msongo wa mawazo utaona mabadiliko yakitokea . B. Madawa mbalimbali  Imekuwa ni desturi sisi kutumia dawa kama diclofenac,aspirin na zingine

FAIDA ZA KIAFYA ZA KULA PILIPILI

14.Pilipili kali.  Watu wengi wamekuwa wakiacha kutumia pilipili etu kwa sababu ya ukali wake. Ila itambulike kuwa ijapokuwa ni kali lakini ila faida nyingi sana kwa afya ya mtu. Pilipili pia ina vitamini c ndani yake kwa kiasi. Vitamini hivi ni muhimu sana katika mfumo mzima wa kinga ya mwili dhidi ya magonjwa na wadudu shambulizi. Pilipili zote zina vitamin A, C na K lakini pilipili nyekundu zimezidi wenzie. Wataalamu wa afya wanazungumza kuwa antioxidant, vitamin A na C vilivyomo kwenye pilipili husaidia katika kuzuia maradhi ya saratani na baadhi ya maradhi yanayohusiana na kuzeheka, na pia husaidia katka kuboresha mfumo wa kinga. Pia vitamin K husaidia katika kuganda kwa damu, kuimarisha mifupa pia husaidia katika kulinda seli. Pilipili nyekundu ni chanzo kizuri cha carotenoid ambayo hutambulika kama lycopene, hii ni mujarabu sana katika kuzuia mwili kupata maradhi ya saratani ya kibofu, njia ya uzazi kwa kinamama na saratani ya kongosho.pia kuna carotenoid inayotambulika k

SIKU YA KUPATA MIMBA

Image

FAHAMU FAIDA ZA MBEGU ZA MABOGA

Image
FAIDA ZA MBEGU ZA MABOGA Zifuatazo ni faida za kiafya ambazo mtu anaweza kuzipata kwa kula mbegu za maboga zikiwa mbichi au zilizo kaangwa: Huimarisha moyo na mifupa. Mbegu za maboga huwa kiwango kingi cha madini aina ya magnesium, ambayo ni muhimu kwa afya ya moyo na uimarishaji wa mifupa pamoja na mishipa ya damu sambamba  na kuongeza ufanisi wa utumbo mpana . Magnesium inaonesha uwezo mkubwa wa kuzuia mshtuko wa moyo na kiharusi.  Kinga ya mwili Mbegu za maboga zina kiwango cha madini aina ya zink, ambayo pia yana faida nyingi mwilini ikiwa ni pamoja na na uimarishaji wa kinga mwilini , ukuaji wa seli, macho na ngozi ya mwili. Hali kadhalika zinki huimarisha nguvu za kiume. Saratani ya kibofu Kutokana na kuwa na kiwango kingi cha zinki, tafiti zinaonesha kuwa mafuta ya mbegu zenyewe za maboga huweza kutumika kama dawa ya kutibu saratani ya kibofu. Ugonjwa wa ini Mbegu za maboga pia zina kamba lishe na kinga kubwa ya kupambana na magonjwa nyemelezi. Mbali na hayo mbe

FAHAMU FAIDA YA KUNYWA MAJI NA KUCHANGANYA NA LIMAO

Image
FAIDA YA KUNYWA MAJI NA KUCHANGANYA NA LIMAO Umesikia mara nyingi kuwa kunywa maji kwa wingi hasa asubuhi kuna faida kubwa sana za kiafya mwilini,lakini kunywa maji yenye ndimu na vuguvugu kuna faida maradufu na ni rahisi kufanya kila siku. Vitamin C nyingi iliyomo katika ndimu (au limao) ni siri ya faida za tunda hili,ukiachia vitamini C ndimu ina vitamini B-complex, madini ya Kalsiamu, chuma, magnesiamu na potasiumu, na fiba (Ndimu ina potasiumu kwa wingi kuliko tofaa (apple au Zabibu). Tunajua kwa watu wengi Kunywa maji peke yake (yasiyo na kitu) wakati wa asubuhi hupata tabu na baadhi ya wengine hupata kichefuchefu . Lakini maji yaliyotiwa ndimu kidogo huwa na radha nzuri zaidi na watu wote wanaweza kunywa bila shida. Faida kubwa ya juisi ya ndimu ni kinga dhidi ya malaria. Kamau glasi moja ya ndimu asubuhi na mapema kabla ya kupiga mswaki na kuinywa. Hakika utakuwa umejijengea kinga dhidi ya malaria. Kisha kila siku asubuhi, kabla ya mswaki uwe na tabia ya kunywa angalau

FAHAMU ZAIDI KUHUSU CHIA

Image
FAHAMU ZAIDI KUHUSU CHIA     Mara nyingi tumekuwa tukiyaangazia masuala mbali mbali ya vitu vinavyotuzunguka. basi Leo siyo vibaya kama tukijaribu kuziangazia afya za wenzetu.     Na katika hili tutaongelea juu ya mbegu ndogo sana ya Chia,ambayo imeendelea Kujipatia umaarufu siku hadi siku hivyo Kuonekana yenye thamani sana hasa kwa Watumiaji wake.     Mbegu za Chia zawezakuwa na rangi Nyeupe ama Nyeusi ikiwa na michirizi ya Mistari mfano wa ramani kwa muonekano.Ikumbukwe kuwa hakuna Tofauti yoyote ya virutubisho kati ya Chia nyeupe na nyeusi.     Mbegu hizi ndogo zipo na mambo mbali mbali na mengi ya kujivunia hasa Kwa watumiaji wake.     Katika miaka ya 3500BC,Chia ilikuwa ni Miongoni mwa vyakula vikuu ktk kabila la Wa Aztec chimbuko lao ikiwa ni Mexico. Baadae miaka ya 1500 na 900BC,Chia ilikuwa tayari inalimwa na makabila mengine(Teotihuacan,Teltec).     Tofauti na wa Aztec makabila haya mawili watu wake waliitumia Chia ktk Matumizi mbali mbali(chakula,vinywaji

FAHAMU FAIDA 10 ZA MAYAI KIAFYA

Image
Mayai ni moja ya vyakula vichache ambavyo naweza kuviweka katika kundi la vyakula ‘bora zaidi’ kuliko vyote. Mayai yamejaa viinilishe muhimu na vingi kati ya hivyo viinilishe havipatikani kirahisi katika vyakula vingi vya kisasa. ZIFUATAZO NI FAIDA 10 ZA KIAFYA ZITOKANAZO NA ULAJI WA MAYAI:- : Mayai yana virutubisho vya kushangaza,Mayai ni moja ya vyakula vyenye virutubisho vizuri zaidi katika sayari dunia. : YAI moja zima lina viinilishe vyote vinavyohitajika kuibadili seli moja kuwa kifaranga cha kuku. Yai moja kubwa lililochemshwa lina: Vitamin A: 6% Folate: 5% Vitamin B5: 7% Vitamin B12: 9% Vitamin B2: 15% Phosphorus: 9% Selenium: 22% : Mayai pia yana kiasi cha kutosha cha Vitamini D, Vitamini E, Vitamini K,Vitamini B6,kalsiamu na Zinki. : Yai moja pia linakuja na kalori au nishati 77,gramu 6 za protini na gramu 5 za mafuta yenye afya au mafuta safi kwa ajili ya mwili (healthy fats). : Mayai pia yana viinilishe vingine vidogo vidogo (trace nutrients) ambav

FAIDA 13 ZA TANGO (CUCUMBER).

Image
ZIPO FAIDA 13 ZA TANGO (CUCUMBER). Mara kadhaa tumekua tukitumia Tango kama moja ya matunda yetu. Lakini je umepata kujua kazi za Tango mwilini? Makala hii itaangazia faida kedekede za Tango katika mwili wa binadamu. Wengi wetu tumekua tukila matunda kwa kupenda ladha yake lakini hatujapata bahati ya kujua kwa undani faida za matunda hayo. Awali ya yote ni vyema kutambua ni tango lipi linafaaa kwa kula? Tango linalofaa kwa kula ni tango lenye rangi ya kijani iliyokolea na lisilo tepeta, tango la aina hii ni zuri zaidi. FAIDA ZA TANGO. 1. Tango husaidia kuupatia mwili maji. Sehemu kubwa ya tunda hili ni maji hivyo basi husaidia kurejesha maji mwilini. 2. Kupunguza sumu mwilini. Kutokana upatikanaji wa maji mengi kwenye tunda hili hvo basi ni rahisi kwa maji haya kusaidia zoezi la kuondosha taka mwilini. 3. Chanzo cha vitamin B. Madini ya silca yapatikananayo kwenye tango husaidia kucha na nywele kung`aa pia kuna madini ya silcon na sulfur kwenye tunda  hili madini h

KITUNGUU MAJI KINAVYOTIBU MAGONJWA MBALIMBALI

Image
KITUNGUU MAJI KINAVYOTIBU MAGONJWA MBALIMBALI Kitunguu maji ni aina ya mboga za majani (vegetable) Viini lishe vilivyomo katika kitunguu maji Vitamini C Penisilini (penicillin) Antiseptic Madini yaliyomo katika kitunguu maji . Salfa,CHUMA,phosphorasi MAGONJWA YANAYOTIBIWA NA KITUNGUU MAJI. magonjwa ya ngozi, (fangasi,upele,ukurutu,mba ,mapunye) Tengeneza juisi ya kitunguu maji kisha paka sehemu yenye matatizo kutwa mala mbili kwa muda wa siku tano utapata majibu mazuri hakika tiba hii ni nzuri sana. Maralia,,,,,,,kula KITUNGUU maji na pili mtama utapona inshaallah KUJITIBU UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA KIKE chukua kitunguu maji kata kata vipande vidogo vidogo  changanya na asali kula mchanganyiko huo hasubui na jion  ndani ya siku Kumi utapata majibu mazuri hakika utakua na nguvu nyingi zaidi. PUMU chukua kitunguu maji kisage kwenye Brenda kisha changanya na asali Matumizi kula vijiko viwili hasubui na jion kwa muda wa siku tano utapata majibu. SARATANI

FAHAMU FAIDA 6 ZA KULA TUNDA CHUNGWA

Image
FAHAMU FAIDA 6 ZIPATIKANAZO KWA KULA TUNDA LA CHUNGWA KIAFYA. Ukiamua kuzungumzia matunda yenye faida ndani ya mwili wa binadamu basi ni lazima utalitaja chungwa kwani lina faida muhimu ikiwemo kujenga kinga imara za mwili. Licha kwamba baadhi ya watu hulitumia tunda hili kama kiburudisho tu bila kujua faida zake mwilini, lakini leo napenda uzifahamu hizi faida  6 unazoweza kuzipata unapokula chungwa iwe chungwa lenyewe au juisi yake halisi. 1. UKOSEFU WA CHOO Kutokana kuwa na kiwango kikubwa cha kirutubisho aina ya kambalishe ‘fibre’, chungwa husaidia usagaji wa chakula tumboni na hutoa ahueni kwa mtu mwenye matatizo ya ukosefu wa choo. 2.HUPUNGUZA HATARI YA MAGONJWA YA MOYO Kiwango kikubwa cha Vitamin C na virutubisho vya ‘flavonoids’, ‘phytonutrients’ vilivyomo kwenye chungwa, huondoa kwa mlaji hatari ya kupatwa na magonjwa ya moyo ‘Cardiovascular disease’ 3. MIFUPA NA MENO Chungwa lina kiasi kingi cha madini ya ‘calcium’ ambayo ni muhimu kwa kuimarishaji afya ya men

FAIDA SABA (7) ZA MDALASINI (CINNAMON)

Image
Mdalasini ni aina ya mmea ambao hutumika kama kiungo kwenye chakula kwani hutia radha madhubuti kutokana na harifu yake nzuri ya kuvutia. Faida zake 1.KUPUNGUZA KOLESTEROLI MBAYA MWILINI. Kolesteroli/lehemu (cholesterol) ni aina ya mafuta/fati (fat) ambayo hupatikana kwenye chembe za damu.kolestroli huwa ni kama nta ambayo wakati mwingine hujishikiza kwenye kuta za mishipa ya damu. Hii ni kwa sababu ya vyakula vyenye mafuta(lipid foods) kama nyama n.k. Hivyo mdalasini hupambana na cholesterol/lehemu aina ya lipoprotini ya chini LDL(Low Density Lipoprotein) ambayo husabaisha shinikizo la damu (hypertension). 2. MDALASINI HUWA NA VIRUTUBISHO MUHIMU KWA MWILI.  Virutubisho hivyo huwa kazi kama kuboresha mifupa na meno kuwa imara zaidi yaani meno huwa na kinga dhidi ya kuoza 3.KUSAIDIA KUPUNGUZA UZITO. Kwa matumizi mfululizo ya mdalasini husaidia kupunguza uzito usiostahili 4. MDALASINI HUWA NA KAZI YA KUBORESHA KIWANGO CHA SUKARI KWENYE DAMU. Kumbuka kiwango cha sukari

KISA CHA MWANAFUNZI ROSE

Image
Kuna mwalimu wa shule ya sekondari alikuwa amezoea kumchapa viboko mwanafunzi mmoja mchelewaji. Mwanafunzi huyu alikuwa akichelewa kipindi cha kwanza kila siku. Hivyo, siku ambazo mwalimu huyu alikuwa na kipindi cha kwanza, mwanafunzi huyu alikuwa anachapwa kwanza kabla ya kuingia darasani. Hali hii iliendelea kwa muda mrefu. Wiki moja ilipita bila yule mwanafunzi kuonekana shuleni. Wiki lililofuata yule mwanafunzi alifika shuleni kabla ya mwanafunzi mwingine yeyote. Mwalimu yule alipomwona alifurahi sana. Alipoingia darasani alimwita yule mwanafunzi na kumsifia sana mbele ya darasa. "Rose, simama. Darasa, Mpigieni makofi "Rose" kwa sababu leo kawa wa kwanza kufika shuleni. Kumbe fimbo zile zimesaidia enhe" Wanafunzi walipiga makofi huku wengine wakimcheka huyo "Rose" Yule mwanafunzi alimwomba mwalimu ampe nafasi aseme jambo. Mwalimu akamruhusu "Mwalimu, siku zote nilizokuwa nikichelewa kufika shule nilikuwa namuuguza mama yangu. Baba yang

πŸ’žπŸ’ž MAUMIVU WAKATI WA TENDO LA NDOA πŸ’žπŸ’ž

Image
Maumivu wakati wa tendo la ndoa (DYSPAREUNIA) si tu huharibu mudi bali hupelekea kumfanya humusika kuchukia/kuogopa tendo lenyewe, kukosa hamu ya tendo lenyewe na kukosa mashirikiano. Maumivu wakati wa tendo au baada ya tendo ni tatizo kubwa linalowasumbuwa baadhi ya wanawake na wanaume ila ukiona ufanyapo tendo La ndoa na kuhisi maumivu basi juwa mwili wako unakupa ishara ya kwamba kuna kitu hakipo sawa na nivizuri kujichunguza ili kujuwa tatizo. πŸ’—πŸ’–Zifuatazo ni hali zinazopelekea kusababisha  na namna ya kulitatuwa hilo tatizo πŸ’•Kutofanyika maandalizi ya kutosha.   Mwanamke kupata hamu huchukuwa muda sana kuliko mwanaume hivo kunatakiwa kuwepo muda wa kutosha ktk suala zima la kutomesana(oral sex), Sio dakika 5 ukishaona majimaji kidogo na kuanza tendo La ndoa hali hii hupelekea kutokea maumivu na kumfanya mtu kuchukia tendo. Unapomuandaa mwenzio vizuri hupelekea damu kutembea vizuri ktk genitals na kufanya kuongezeka majimaji ktk uke (lubrication) yatakayopelekea kulainisha

MKE WANGU SAMAHANI (FULL STORY)

Image
MKE WANGU SAMAHANI             (FULL STORY) Asubuhi aliamka na kumkuta mkewe akisali. Akamsikia mkewe akimuombea. Akamtazama kwa sekunde kadhaa. Ni muda mrefu sana tokea amemshuhudia mkewe akisali. Wamekuwa na ugomvi na kutoelewana katika ndoa yao Kwa miezi kadhaa sasa. Usiku wa jana yake wamegombana ugomvi mkubwa mno. Haraka haraka Mume akainuka kitandani na kuelejea jikoni kuandaa kifungua kinywa. Kwa hio miezi kadhaa ya ugomvi mkewe amekua hamuandalii chakula. Kwa mshangao, akakuta staftahi imeshaandaliwa mezani. Akala. Baada ya kumaliza akarudi chumbani, kujiandaa aingie bafuni. Mke nae akawa anatoka bafuni. "Habari za asubuhi. Uwe na siku njema". Mke akamsalimia mumewe na kumtakia kazi njema, huku wakipishana bafuni Baada ya kuoga, na kuvaa tayari kwenda kazini; akamuona mkewe jikoni, akila staftahi akiwa na amani. Alikuwa akila kifungua kinywa huku akicheka kutokana na kuangalia video za vichekesho alizotumiwa WatsApp. Mume akamtizama kwa dakika kadhaa ha

KITUNGUU SWAUMU NA NA FAIDA ZAKE MWILINI

Image
KITUNGUU SWAUMU NA NA FAIDA ZAKE MWILINI +255 716 737 730 Kitunguu swaumu hutibu magonjwa 30 Haya ni baadhi ya magonjwa yaliyothibitika kutibika na yanatibika au kukingika na kitunguu swaumu: 1. Huondoa sumu mwilini 2. Husafisha tumbo 3. Huyeyusha mafuta mwilini (kolestro) 4. Husafisha njia ya mkojo na kutibu U.T.I 5. Hutibu amoeba, minyoo na Bakteria wengine 6. Huzuia kuhara damu (Dysentery) 7. Huondoa Gesi tumboni 8. Hutibu msokoto wa tumbo 9. Hutibu Typhoid 10. Huondoa mabaka mabaka kwenye ngozi 11. Hutibu mafua na malaria 12. Hutibu kifua kikuu (ukitumia kitunguu swaumu kesho yake unaweza kutokwa na makohozi mengi tu ambayo ni ishara kwamba kweli kinatibu kifua kikuu (TB) 13. Hutibu kipindupindu 14. Hutibu upele 15. Huvunjavunja mawe katika figo 16. Hutibu mba kichwani 17. Huupa nguvu ubongo. Kazi nzuri niliyopenda zaidi katika kitunguu swaumu. 18. Huzuia meno kung'ooka na kutuliza maumivu 19. Huongeza SANA nguvu za kiume pia hutibu uanithi (kush

FAIDA 14 ZA MAEMBE KIAFYA.

Image
FAIDA ZA MAEMBE KIAFYA.  Maembe ni matamu sana kiradha na hupendwa na watu katika hali toauti. Mtu anaweza akawa mgonjwa lakini hamu yake ikawa ni maembe kwan wakat mwingine huwa yanarudisha hamu ya kula pale ujisikiapo mgonjwa na kukosa hamu ya chakula.  FAIDA ZA KIAFYA ZA MAEMBE NI HIZI.  1. Husaidia sana katika mfumo wa mmeng'enyo wa chakula.  Huongeza nguvu katika usagaji wa chakula tumboni.  2. Huzuia na kupambana na saatani/ kansa.  Hii ni kwa sababu maembe huwa na viua sumu kama quercetin, fisetin, astragalin, gallic acid, methyl gallate na isoquercitrin ambazo hupambana sana na kansa ya matiti, colon cancer na prostate cancer/kansa ya kibofu.  3 Husawazisha kiwango cha cholesterol/lehemu kuwa katika mstari usio na hatar ya kupata kisukari.  Kumbuka hii pia ni kaz ya majani ya maembe. Uwepo wa vitamin C, fibres/kamba au nyuz lishe na madini kama chuma/iron. Chuma majani sita hadi tisa, chemsha kunywa asubuhi kabla ya kula chochote. 4. Kuongeza uzito

adthis