FAHAMU FAIDA 10 ZA MAYAI KIAFYA




Mayai ni moja ya vyakula vichache ambavyo naweza kuviweka katika kundi la vyakula ‘bora zaidi’ kuliko vyote.

Mayai yamejaa viinilishe muhimu na vingi kati ya hivyo viinilishe havipatikani kirahisi katika vyakula vingi vya kisasa.

ZIFUATAZO NI FAIDA 10 ZA KIAFYA ZITOKANAZO NA ULAJI WA MAYAI:-
:
Mayai yana virutubisho vya kushangaza,Mayai ni moja ya vyakula vyenye virutubisho vizuri zaidi katika sayari dunia.
:
YAI moja zima lina viinilishe vyote vinavyohitajika kuibadili seli moja kuwa kifaranga cha kuku.
Yai moja kubwa lililochemshwa lina:
Vitamin A: 6%
Folate: 5%
Vitamin B5: 7%
Vitamin B12: 9%
Vitamin B2: 15%
Phosphorus: 9%
Selenium: 22%
:
Mayai pia yana kiasi cha kutosha cha Vitamini D, Vitamini E, Vitamini K,Vitamini B6,kalsiamu na Zinki.
:
Yai moja pia linakuja na kalori au nishati 77,gramu 6 za protini na gramu 5 za mafuta yenye afya au mafuta safi kwa ajili ya mwili (healthy fats).
:
Mayai pia yana viinilishe vingine vidogo vidogo (trace nutrients) ambavyo ni mhimu kwa afya bora.
:
Hakika…mayai ni chakula ambacho ni karibu kimejikamilisha,mayai yana karibu kila aina ya kiinilishe muhimu tunachokihitaji kila siku.
:
EPUKA PROPAGANDA KUWA UKILA MAYAI UTAPATA MARADHI FLANI,MWANGALIE JIRANI YAKO KAKATAZWA KULA MAYAI KWA SABABU YA MARADHI FLANI LKN MPAKA LEO ANAUMWA JAPOKUWA AMEACHA KILA MAYAI.

Comments

adthis

Popular posts from this blog

FAIDA ZA PILIPILI MANGA KIAFYA

FAHAMU FAIDA 10 ZA NAZI KAMA TIBA YA MWILI