Posts

Showing posts from March, 2024

JE! NINI HUSABABISHA WANAWAKE VIUNO VYAO KUUMA??

Image
Maumivu ya kiuno kwa wanawake huwa yana sababu nyingi. Mengine yanahusiana na hali maalumu kwa wanawake, huku mengine yanaweza kujitokeza tu kwa mtu yeyote. Katika makala hii tutaangalia visababishi vya maumivu ya kiuno kwa wanawake, hivyo kila mmoja mwenye tatizo hili ataona umuhimu wa kwenda kupima na kuweza kupata matibabu. Je, Nini Husababisha Kiuno Kuuma? Baadhi ya visababishi vya maumivu ya kiuno kwa wanawake hutokana na hali maalumu, nazo zipo kama ifuatavyo; 1. Ugonjwa Wa Kabla Ya Hedhi(PMS) Hii huwa ni hali ambayo wanawake wengi huipata kabla ya vipindi vyao vya hedhi. Hali hii ina dalili nyingi, lakini hutaziona zote. Kwa kawaida dalili hizi huwa kama hivi; a) Dalili Za Mwili, kama vile; •Maumivu ya kiuno • Kichwa kugonga • Uchovu • Tumbo kuunguruma b) Dalili Za Kihisia Na Kitabia, kama vile; • Kubadilika badilika kwa hali ya moyo • Kutamani vyakula • Wasiwasi • Shida kuzingatia • Kujikita kwenye tatizo Ugonjwa wa kabla ya hedhi(Premenstrual Syndrome au PMS) huanza siku chach

FAIDA ZA GANDA LA NAZI KIAFYA

Image
  FAHAMU FAIDA ZA GANDA LA NAZI(COCONUT HUSK) hutibu typhoid. husafisha Ini Husafisha figo Husafisha damu Huimarisha afya ya ngozi. Chukua ganda la Nazi.osha vizuri kwa nje.loweka kwenye maji kiasi kwamba lizame lote ndani ya maji.Acha kwa siku mbili.chuja maji Yake na utunze kwenye chombo safi. Matumizi. Mtu mzima anywe kikombe kimoja kubwa Mara mbili. Mtoto atumie vijiko 2 vya chakula kutwa Mara 2 kwa siku 14.

FAIDA 5 ZA KIAFYA KUTUMIA MCHAICHAI KAMA

Image
FAIDA YA KUTUMIA MCHAICHAI KAMA TIBA NA CHAKULA Faida za mchachai zipo nyingi sana wengi wetu hudhani mchaichai ni kuongo cha kuweka kwenye chai pekee,au ni dawa kwa ajili ya kuua mbu pekee,ila mchaichai huwa na faida lukuki zaidi ya hizo tu. Naomba uweze kusoma makala haya ili uone faida nyinginezo za mchaichai. faida za mchaichai kiafya. 1. Mchaichai ni kinga dhidi ya saratani. Tafiti mbalimbali zimeonyesha kuwa kwenye kila gram 100 ya mchaichai, kuna viondosha sumu ambavyo vina uwezo wa kuukinda mwili dhidi ya ugonjwa wa saratani. Mwaka 2006, timu ya watafiti kutoka Chuo kikuu cha Gurion, Israel waligundua mchaichai una uwezo wa kuua seli zinaweza kusababisha saratani. 2. Hutibu magonjwa ya kuhara. Husaidia umeng’enyaji wa chakula Chai ya mchaichai hurahisisha utaratibu wa mmeng’enyo wa chakula na pia hutibu magonjwa ya kuhara na maumivu ya tumbo ikiwamo kujaa gesi. Hurahisisha utaratibu wa kuondoa uchafu mwilini Katika matibabu, unatibu magonjwa mengi ikiwemo kushusha joto, hasa kw

ZIJUE FAIDA ZA 15 ZA MAJANI YA MRONGE

Image
  ZIJUE FAIDA ,TIBA NA VIRUTUBISHO MBALIMBALI VINAVYO PATIKANA KWENYE MTI WA MRONGE.. 1:inajumala ya virutubisho92    2:viondoa sumu46,   3:huondo mafuta mwilini  4:viondoa uvimbe36  . 5: huongeza CD4 cell(white blood cell)   6:ina kiasi Cha kutosha Cha madini ya zink ambayo hutumika kuongeza nguvu zakiume  7:mronge huupa Mwili nguvu kupata hamu ya kula  8:hutibu zaidi ya maradhi 300 ikiwepo presha,sukari ,vidonda vya tumbo,pumu ,nguvu zakiume,u.t.i sugu,kuhara, kusafisha mirija ya uzazi.   9: mronge una vitamin c ambayo Ni mara7 ya vitamini c inayopatikan katika machungwa ambayo husaidia Kinga ya Mwili dhidi ya magonjwa,husaidia katika utengenezaji na uimara wa mifupa,meno misuli na ngozi,husaidia kutoa kikohozi na mafua ya alegy   10: mronge una madini ya chuma ambayo Ni Mara 17 ya madin yachuma yanayopatikana katika maziwa ambayo husaidia kuzalisha homoni katika mwili wa binadam ambazo hufanya kazi mbali mbali mbali Kama kuhakikisha kiwango Cha sukari mwilini kipo sawa pia husaidia

KWANINI UTI INAWASUMBUA SANA WANAWAKE KULIKO WANAUME??

Image
  KWA NINI UTI INAWASUMBUA WANAWAKE ZAIDI KULIKO WANAUME? UTI (Urinary tract infection) ni ugonjwa wa maabukizi katika mfumo wa mkojo na maambukizi haya yanasababishwa na bakteria aitwaye Escherichia coli.   Kwa kawaida bakteria hawa hupatikana katika utumbo mpana na kwenye njia ya haja kubwa na inapotokea wakahamia katika njia ya mkojo husababisha mtu kupata tatizo hili la maambukizi katika mfumo wa mkojo. Ugonjwa wa U.T.I unaweza athiri urethra, kibofu cha mkojo na figo. DALILI ZA UTI ➢ Kwenda haja ndogo mara kwa mara na maumivu wakati wa kukojoa ➢ Kuhisi kuunguzwa na mkojo kwenye kibofu au mrija wa mkojo ➢ Maumivu chini ya kitovu. ➢ Mkojo kuwa na harufu mbaya na pia kubadilika rangi kuwa nyeusi au rangi ya mawingu. ➢ Kuhisi homa kali na uchovu na kichefuchefu. ➢ Kushikwa na hamu ya kukojoa ila mkojo unatoka kidogo. ➢ Maumivu ya mgongo na kiuno.  ➢ Uchovu kupita kiasi wa mwili mzima.  ➢ Kupata hamu kubwa ya kwenda haja ndogo lakini inatoka kiduchu.  ➢ Haja ndogo kutoka legevu au lege

FAHAMU FAIDA ZA KITUNGUU SWAUMU

Image
  Inasaidia kuyeyusha mafuta mwilini. 🧄 Inasaidia kusafisha njia ya mkojo  na inasaidia kupunguza kasi ya uweneaji wa maambukizi hasa magonjwa kama Fangas, PID, UTI na magonjwa ktk  mfumo wa chakula.  🧄 inasaidia kupunguza maumivu ya jongo \Gout 🧄 Inaongeza hamu ya kula  🧄 inasaidia kuzuia saratani 🧄 Inasaidia kuongeza kinga mwilini kwa kuongeza uzalishaji seli mpya idadi nyingi . 🧄Inazuia magonjwa kama typhoid, kuhara damu na msokoto wa tumboni na kipindupindu 🧄 Inasaidia kuondoa mabaka mabaka  kwenye ngozi 🧄kitungu swaumu inasaidia kupunguza athari za msongo wa mawazo na kutibu changamoto ya kukosa usingizi. Kitungu swaumu kinasaidia kuupa ubongo nguvu na afya yakufanya kazi vizuri 🧄 Inasaidia kuongeza nguvu za kiume, wababa hii nawakikishia kabisa. 🧄 Inasaidia kuongeza kasi ya mmeng'enyo wa chakula tumboni . 🧄 Inasaidia kupunguza maumivu ya kichwa 🧄 Inasaidia kupunguza madhara ya Kisukari (Dm) *MATUMIZI YA VITUNGU SWAUMU*  Tumia vitungu swaumu punje 5 Asubuhi, mchana

ZUJUE SABABU ZA TUMBO KUJAA GESI

Image
Chakula kutokusagwa au mchafuko wa tumbo ni msemo wa kawaida ambao huelezea masumbufu ndani ya tumbo lako la juu. Chakula kutokusagwa sio ugonjwa, bali kuna baadhi ya dalili unaweza kuzipata, ikiwa pamoja na maumivu ya tumbo na kujisikia tumbo kujaa gesi muda mfupi tu unapoanza kula. Ingawa hali ya tumbo kujaa gesi huwa ni ya kawaida, lakini kila mtu anaweza kupatwa na hali ya kukosa choo katika njia tofauti. Dalili za tumbo kujaa gesi unaweza kuzihisi mara kwa mara au kila siku. Je, Dalili Zake Zinakuwaje? Watu wenye tatizo la tumbo kujaa gesi kwa karne hii ni wengi sana, na dalili zake huwa kama hivi ifuatavyo; • Tumbo kujaa haraka tu wakati unapokula hata kama ni chakula kidogo • Kutokujisikia vizuri baada ya kumaliza kula • Kuhisi masumbufu kwenye tumbo la chakula • Kuhisi kama hali ya kuwaka moto maeneo ya tumbo la juu • Tumbo kuunguruma • Kuhisi kichefuchefu NUKUU: Wakati mwingine watu wenye tatizo hili pia huhisi kiungulia, lakini kiungulia na tumbo kujaa gesi ni hali mbili zina

adthis