FAHAMU FAIDA ZA KITUNGUU SWAUMU

 




Inasaidia kuyeyusha mafuta mwilini.

🧄 Inasaidia kusafisha njia ya mkojo  na inasaidia kupunguza kasi ya uweneaji wa maambukizi hasa magonjwa kama Fangas, PID, UTI na magonjwa ktk  mfumo wa chakula. 


🧄 inasaidia kupunguza maumivu ya jongo \Gout


🧄 Inaongeza hamu ya kula 

🧄 inasaidia kuzuia saratani


🧄 Inasaidia kuongeza kinga mwilini kwa kuongeza uzalishaji seli mpya idadi nyingi .


🧄Inazuia magonjwa kama typhoid, kuhara damu na msokoto wa tumboni na kipindupindu


🧄 Inasaidia kuondoa mabaka mabaka  kwenye ngozi


🧄kitungu swaumu inasaidia kupunguza athari za msongo wa mawazo na kutibu changamoto ya kukosa usingizi. Kitungu swaumu kinasaidia kuupa ubongo nguvu na afya yakufanya kazi vizuri


🧄 Inasaidia kuongeza nguvu za kiume, wababa hii nawakikishia kabisa.


🧄 Inasaidia kuongeza kasi ya mmeng'enyo wa chakula tumboni .


🧄 Inasaidia kupunguza maumivu ya kichwa


🧄 Inasaidia kupunguza madhara ya Kisukari (Dm)



*MATUMIZI YA VITUNGU SWAUMU* 


Tumia vitungu swaumu punje 5 Asubuhi, mchana punje5 na punje 5 jioni. Meza kama vidonge na kunywa maji ya kawaida au vuguvugu angalau kikombe kikubwa cha maji chenye ujazo wa mls 400. 


Mtu mwenye changamoto ya Pressure ya kushuka na mwenye vidonda vya tumbo haruhusiwi kutumia vitungu swaumu hata kidogo.


Vitungu swaumu kama punje zake ni kubwa kata punje ndogo ndogo sana angalau kumi meza kwa mara moja ili kupata urahisi wa kumeza .


Mama mjamzito sio salama sana kutumia vitungu swaumu. Na kama anataka kutumia weka kwenye mboga.


 *MADHARA YA VITUNGU SWAUMU* 


🧄Huleta harufu mbaya Mdomoni hasa pale unapotumia kwa kutafuna. Lakini hii unaweza kuondoa harufu kwa kunywa maziwa angalau kikombe kimoja cha ujazo wa 250mls,kunywamaji mengi, na kutafuna karafu. 


🧄 Inasababisha mzio au Mcharuo mwilini (Allergies au Inflammatory reaction)


🧄Vinaleta kichefuchefu, kutapika, au kuharisha. Ikitokea umeharisha badaa ya kutumia kitungu swaumu ni vizuri maana ni njia mmoja wapo ya kuondoa uchafu uliokuwepo tumboni japo ni wachache sana wanapata hii hali.


Katika watu kumi 10 watakao tumia hali hii inaweza kuwapata watu  1hadi 3.


🧄 husababisha kuvuja damu zaidi, ukiwa  na jeraha au period maana huzuia au hupunguza hufanyaji kazi wa seli sahani platelets ambazo ni mahususi kwa kugandisha damu. Ndio maana mama mjamzito na mama aliyejifungua wanatumia kwa special case na sio lazima wao kutumia bali kuna mbadala wake .


🧄Vitungu swaumu huwa vina mwingiliano na badhii ya dawa kama vile Warfarin, Antiplatelets, saquinavir, calcium channel blockers na Antibiotics jamii ya quinolone kama vile ciprofloxacillin.

Comments

adthis

Popular posts from this blog

FAIDA ZA PILIPILI MANGA KIAFYA

FAHAMU FAIDA 10 ZA NAZI KAMA TIBA YA MWILI