FAIDA ZA PILIPILI MANGA KIAFYA

PILIPILI MANGA / BLACK PEPPER:

Kiungo hiki kizuri kwa mwanamke ambaye amejifungua au mimba imeharibika na yupo kwenye utaratibu wa kuondoa uchafu usibakie kwenye kizazi.
  Tumia Uji uliotiwa Pilipili manga sio chini ya siku 21.......

KWA FAIDA YA WOTE:
Pilipili manga mara nyingi hutumika kama kiungo kwa ajili ya kuongeza ladha kwenye chakula.
Lakini kiungo hicho kina faida kadhaa kiafya mwilini ambazo unapotumia unapaswa kuzijua faida zake kwa sababu ina wingi wa madini ya Manganizi, Shaba, Magnesiamu, Kalsiamu, Fosforasi, Chuma na Potasiamu.

Vitamini: Pilipili manga ina wingi wa Vitamini B2, Vitamini B6, Vitamini C na Vitamini K.
Vilevile pilipili manga ina winga wa Nyuzi lishe, Protini na wanga.

~Uwepo wa virutubisho hivi ni muhimu kwa ajili ya mmeng'enyo wa chakula kwa wenye matatizo ya choo na tumbo kujaa gesi

~Kupunguza uzito.
Magamba ya nje ya pilipili manga yanasaidia sana katika kuvunjavunja seli za mafuta mwilini.
Seli hizo huvunjwavunjwa na kutumika katika matumizi mengine ya mwili kitu kinachoifanya pilipili manga kuwa njia nyingine mbadala ya kupunguza mafuta mwilini.

>>Tiba ya kifua na mafua.
Kwa mafua ya kawaida na kikohozi pilipili manga ni tiba nzuri ya asili.

>>Kuondoa sumu mbalimbali mwilini.
Pilipili manga ina viondoa sumu ambavyo husaidia kuondoa sumu mbalimbali mwili ambazo zinaweza kuleta madhara mfano saratani, pia kupunguza kasi ya mwili wako kuchoka na kuonekana mzee kabla ya umri na kupunguza kasi ya kupoteza kumbukumbu ikiwemo kuboresha ufyonzaji wa virutubisho vingine mwilini.

>>Ni msaada kwa wenye tatizo la pumu (Asthma)
Kutokana na kuwepo kwa viondoa uchochezi (anti-inflammatory) kwenye pilipili manga, husaidia sana katika matatizo ya mfumo wa hewa kama vile Asthma.
Mengineyo:

ANGALIZO:
<<>>Pilipili manga inaweza kukusababishia chafya.
<<>>Kwa mgonjwa ambaye amefanyiwa upasuaji wa tumbo epuka kuweka pilipili manga nyingi kwenye chakula.
Na kama utatumia pilipili manga ukaona dalili zozote za mzio (Allergy.) acha kutumia muone daktari.

Una tatizo la Afya Ya Uzazi na ungependa kupata msaada zaidi...!

Karibu virutubisho kwa ajili ya kubalansi homoni, kuondoa matatizo ya hedhi, kutibu mayoma, endometrium, ovarian cysts, chango la uzazi, mirija kuziba na mengineyo mengi.

Comments

  1. Naweza kutumia bila kusaga au ni mpaka isagwe

    ReplyDelete
  2. Asanten cn mungu atawalipa inshaa allah

    ReplyDelete

Post a Comment

adthis

Popular posts from this blog

FAHAMU FAIDA 10 ZA NAZI KAMA TIBA YA MWILI