FAHAMU FAIDA SITA ZA UKWAJU KAMA TIBA YA MWILI.



FAHAMU FAIDA SITA ZA UKWAJU KAMA TIBA YA MWILI.

Ukwaju ni tiba ya magonjwa mbalimbali, leo tujaribu kuona faida zake

Majani ya ukwaju yanatibu fangasi, kusafisha kibofu cha mkojo na kutibu maumivu ya viungo.



Magome na mizizi yanatibu tatizo la kukosa choo, matatizo ya tumbo na tumbo kujaa gesi.

Tunda la ukwaju huondoa kemikali sumu, lehemu mwilini na kutibu tatizo la mmeng'enyo, pia inaua bacteria na kuzuia wadudu wasikae katika ngozi.

Ukwaju hutibu homa za mara kwa mara

MATUMIZI
Kunywa juice ya ukwaju usiweke kabisa sukari wala juisi yako usiisage kwa blenda

Kwa ajili ya kuunga sehemu iliyovunjika fanya kuchukua juisi ya ukwaju changanya na mafuta ya ufuta weka jikoni ipate uvuguvugu kisha toa jikoni, chukua dawa uliyoiandaa kandia sehemu iliyovunjika asubuhi na jioni kwa muda wa siku saba utapata matokeo mazuri.

1.KUTIBU NGIRI

Chemsha majani ya ukwaju kunywa kutwa mara tatu kwa siku sita utaona matokeo

2.KUTIBU MAUMIVU YA SIKIO

juisi ya ukwaju maumivu yatakata.
Kuwashwa mwili au vipele mwilini.
Pondaponda majani ya ukwaju, pakaa sehemu yenye matatizo utapata nafuu mapema

3.MWILI KUTOA HARUFU MBAYA.
Chukua ukwaju ulainishe vizuri kisha pakaa kwapani, sehemu za siri na sehemu zozote zinazoa harufu kwenye mwili wako

4.KUPUNGUZA UZITO NA UNENE.
Juisi ya ukwaju kila asubuhi nawe utapunguza uzito na unene.

5.UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME.
Kunywa juisi ya ukwaju asubuhi na jioni ndani ya siku 14 utaanza kupata raha ya tendo la ndoa

6.KUTEGUKA
Chukua juisi ya ukwaju changanya na chumvi ya mawe kisha pakaa sehemu iliyoteguka ndani ya siku tano utapata nafuu kubwa inshaallah.

Ukwaju una faida nyingi sana ndani ya mwili wa binadamu kwa hiyo tunashauriwa kutumia juisi yake bila sukari, majani yake na mizizi yake mara kwa mara sababu ukwaju unatukinga na magonjwa mbali mbali.


Post nyingine bora kwa ajili yako


  1. Magonjwa hatari na afya

  2. Hadithi tamu na za kusisimua

  3. Mkala maalumu za dini

  4. Jifunze kutoa huduma ya kwanza

  5. Makala za sayansi na teknolojia

  6. Masomo ya Shule na mitihani

  7. Chemsahabongo

  8. Faida za mboga na Matunda

Comments

adthis

Popular posts from this blog

FAIDA ZA PILIPILI MANGA KIAFYA

FAHAMU FAIDA 10 ZA NAZI KAMA TIBA YA MWILI