Posts

Showing posts from January, 2020

KISA CHA MFUGAJI NA FARASI WAKE.

Image
Mfugaji mmoja alikuwa anafuga farasi na kondoo, alimtumia farasi kwa usafiri wake.  Siku moja farasi wake aliugua akaamua kumtafuta daktari wa mifugo amtibu haraka. Daktari wa mifugo akajaribu kumpatia dawa, akamwambia mfugaji kuwa ile dawa lazima iwe imemtibu farasi ndani ya siku 5 na kama zitafikia siku 5 hajapona basi itabidi achinjwe maana ni ishara tosha kuwa hatapona tena sababu ya mashambulizi makubwa ya bakteria. Daktari Akaondoka kwa ahadi ya kurudi tena kuangalia maendeleo ya farasi.  Kondoo alikuwa pembeni akisikiliza kwa makini mazungumzo yao.  Siku ya pili ilipofika, kondoo akamfuata farasi akamwambia "jitie nguvu rafiki yangu amka kama sivyo watakuchinja." Lakini farasi hakuwa na nguvu, alishindwa kabisa kuamka. Ikafika siku ya tatu, kondoo akarudia tena kumwambia : "Amka rafiki. yangu, sitaki kuona unachinjwa, jikaze na mimi nitakusaidia kukushika usianguke, haya twende! Moja mbili tatu….." Jitihada za kondoo zikawa bure maana farasi hakuwez

ZIFAHAMU FAIDA ZA NJEGERE KIAFYA

Image
ZIFAHAMU FAIDA ZA NJEGERE(GREEN PEAS) KIAFYA Njegere ni moja ya mmea mithili ya maharage ambayo hutumika kama mboga hasa ikiwa mbichi, rangi yake ni kijani. FAIDA ZAKE 1. HUZUIA MWILI USISHAMBULIWE NA MAGONJWA SUGU. Njegere huwa na virutubisho na nyuzi (fibres). Hivyo magonjwa kama kansa, magonjwa ya moyo na kisukari hukosa upenyo wa kushambulia mwili

UMUHIMU WA KOKOTO KUTANDAZWA KWENYE RELI

Image
Kusafiri ndani ya treni (garimoshi) kuna  upekee wake. - Moja ya kitu cha  pekee utakachokiona ni mawe madogo madogo(kokoto) kuzunguka reli ambapo treni inapita. - Lakini umewahi kujiuliza kwanini reli imetandazwa kokoto hizo? 1- Mawe ya relini yanafanya kazi nyingi. Kwanza kabisa, yanasaidia reli kukaa mahali pake wakati treni yenye uzito mkubwa ikiwa inapita - 2- Pia yanazuia aina yoyote ya majani yasiote karibu na reli ambayo yanaweza kuufanya udongo uliopo chini ya reli kuwa dhaifu na kushindwa kuhimili uzito wa reli na treni - 3- Kazi nyingine muhimu inayofanywa na mawe ya relini ni kuzuia maji yasikusanyike au kukaa muda mrefu kwenye reli na kudhoofisha njia ya reli - Hivyo basi ni jukumu letu sote kulinda na kuhakikisha mawe hayo hayaondolewi kwenye reli kwasababu yamewekwa kwasababu maalumu ya kuimarisha reli na kuwalinda watu wanaotumia usafiri wa treni...

FAIDA 28 ZA MAPERA NA MAJANI YAKE

Image
FAIDA 28 ZA MAPERA NA MAJANI YAKE Mapera ni matunda yanayopatikana kwa wingi lakini mara nyingi huwa hayapendwi sana kutokana na ugumu wake wakati wa kuyatafuna pamoja na kuwa na mbegu mbegu nyingi. Hata hivyo matunda haya yana faida kubwa sana kwa afya ya mwili wa mwanadamu. ZIFUATAZO NI FAIDA KUMI ZA MAPERA. 1. Utajiri wa Vitamin C: Mapera ya utajiri mkubwa wa Vitamin C ambayo ni muhimu sana katika mwili wa mwanadamu. 2. Ni kinga nzuri ya kisukari. Ulaji wa watu wengi unawaweka katika hatari ya kupatwa na ugonjwa wa kisukari lakini matumizi ya mapera yatakupunguzia hatari ya kupatwa na ugonjwa wa kisukari Hii ni kwa sababu mapera yana utajiri mkubwa sana wa Fibre. Fibre ni muhimu sana katika kupunguza kiasi cha sukari kwenye damu. Vilevile ni muhimu sana katika kuusafisha mfumo wa usagaji 3. Kuimarisha Uwezo Wa Kuona Mapera yana utajiri mkubwa sana wa Vitamin A au Retinol ambayo ni muhimu sana katika kusaidia kuona vizuri. Hivyo basi kama ilivyo kwa karoti, mapera

FAHAMU YA KWAMBA MBEGU ZA MPAPAI

Image
Ndugu yangu msomaji fahamu ya kwamba mbegu za mpapai zinatibu magonjwa mengi kwa mtu mwenye kujua kuzitumia. NAMNA YA KUZIANDAA:- Utazichukua mbegu za mpapai utazianika ndani mpaka zikauke hakikisha zisipatwe na mwanga wa jua, zikikauka utazitwanga kisha utazichekesha unga wake utauhifadhi kwa ajili ya kutumia,utatumia kwa maradhi haya yafuatayo:- TIBA YA KISUKARI:- Utakoroga uji mwepesi kikombe kimoja kisha utaweka unga wa mbegu za papai vijiko viwili vya chakula utakua unakunywa asubuhi na jioni kikombe kimoja asubuhi kingine jioni utaendelea na tiba hii hata kwa muda wa wiki mbili mpaka utaona mabadiliko.hii ni Tiba nzuri sana. TIBA YA KIDONDA: Ikiwa mtu anakidonda katika mwili wake anatakiwa akioshe kisha anyunyizie unga wa mbegu za mpapai asubuhi na jioni kitapona haraka. TIBIA YA KIKOHOZI Ikiwa mtu ana kohoa basi achukuwe kijiko kidogo cha unga wa mbegu za papai awe anabwiya asubuhi na jioni kwa muda wa wiki au achukuwe kijiko kimoja atie kwenye kikombe cha

FAIDA 9 ZA KIAFYA ZA TANGAIZI

Image

adthis