MAJANI YA MPERA NA FAIDA ZAKE MWILINI.

 




MAJANI YA MPERA NA FAIDA ZAKE MWILINI.


1. Chai ya majani ya mpera inaponyesha kifua na

kikohozi.


2. Majani ya mpera yaliyosagwa vizuri

yanatumika kutibu muwasho uliotokana na mzio

(allergy).


3. Pia majani haya ya mpera yakichemshwa

kama chai yanaondoa cholesterol iliyozidi

mwilini.


4. Chai ya majani ya mpera inapunguza kiwango

cha tatizo la sukari mwilini.


5. Chai ya mpera ni dawa nzuri kwa wenye

matatizo ya nguvu za kiume.


6. Pia inatumika kama scrub ya uso.

Chukua majani ya mpera saga kisha tia maji kiasi

na inasaidia kuondoa uchafu usoni.


7. Pia majani ya mpera yakichemshwa ni dawa

ya kuponyesha tumbo la kuhara.


8. Kama umejikata kidogo unaweza kutumia

majani ya mpera yalioshwa na kusagwa vizuri

kwa kupunguza maumivu na kukulinda na

maambukizi ya bakteria.


9. Majani ya mpera yaliyosagwa vizuri

yanatumika kutibu eneo la mwili lililong'atwa na

mdudu na kupunguza maumivu.


10. Chai ya majani ya mpera inaaminika kuwa ina

uwezo wa kutibu tezi dume.


11. Kutokana na kuwa na vitamini C kwa wingi

majani ya mpera yana uwezo mkubwa wa kutibu

chunusi.


12. Chai ya majani ya mpera inasaidia kupunguza

uzito mwilini na kuzuia uharibifu sukari ndani ya

mwilini.


13. Majani ya mpera yanajaza nywele na

kurefusha nywele kwa watu wenye tatizo la

kukatika kwa nywele, unasaga na kuchemsha

kisha acha yapoe ndio upake kichwani kutoka

chini ya ngozi ya kichwa hadi kwenye ncha ya

nywele zako.


14. Ukiwa na tatizo la vidonda kwenye ufizi,

maumivu ya jino na ufizi tafuna majani ya mpera

na utaona maajabu ya majani haya.


15. Chukua majani ya mpera saga vizuri mpaka

yawe laini kabisa ongeza na maji kidogo kisha

tumia kupaka usoni kama scrub inatibu ngozi

inayoanza kuzeeka mapema.


16. Chai ya mpera inasaidia kwa kutibu

mvurugiko wa tumbo.


Pamoja na majani hayo kuwa msaada wa kutibu

maradhi mbalimbali , halikadhalika juisi ya

mapera nayo husaidia sana kutibu mgolo au

bawasiri, figo na hata kuondoa mafuta katika

moyo.


Kimsingi mti wa mpera karibu kila sehemu yake

ni tiba kwani hata mizizi yake inapochemshwa na

kutumia kwa kunywa huenda kuwasaidia

wanawake wenye matatizo ya hedhi au wenye

matatizo ya kutokwa na maji yenye harufu

mbaya sehemu zao za siri.


AHSANTENI SANA.....

Comments

adthis

Popular posts from this blog

FAIDA ZA PILIPILI MANGA KIAFYA

FAHAMU FAIDA 10 ZA NAZI KAMA TIBA YA MWILI